
Makundi ya kutetea maslahi ya
wanawake yameghadhabishwa na mahakama ya rufaa nchini Afghanistan ambapo
imebatilisha hukumu ya kifo dhidi ya wanaume wanne waliohusika na
mauaji ya mwanamke mjini Kabul mwezi Machi.
Wakili wa familia ya
mwanamke huyo amelalamikia mahakama hiyo kwa kuendesha uwamuzi wake
faraghani. Naye kakake marehemu amesema uwamuzi huo ni ukiukaji mkubwa
wa haki.
Mwanamke huyo kwa jina Farkhunda, alishambuliwa katika msikiti mmoja baada ya kutuhumiwa bila ukweli kwamba aliiteketeza Koran. Alipigwa mawe hadi kufa, maiti yake ikakanyagwa kwa gari na kisha ikateketezwa.
Mahakama ya rufaa pia imemuachia huru msimamizi wa msikiti huo.


0 Response to "TUKIO LINGINE......Ghadhabu baada ya wauaji kuachiwa huru"
Post a Comment